Tuesday, January 31, 2017

MAKALLA ATOA SIKU 14 KWA HALMASHAURI ZOTE MKOANI MBEYA KUWAONDOA WALIOVAMIA MAENEO YA HIFADHI

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akizungumza na waanchi wa kijiji Cha Hanzya Kata ya Itagano jijini Mbeya katika kilele cha Kampeni ya Upandaji MitiKimkoa  .


Na Emanuel Madafa,Mbeya

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla ametoa siku 14  kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mbeya kuhakikisha inawaondoa watu wote waliovamia maeneo ya hifadhi za misitu pamoja na hifadhi ya misitu ya mlima Mbeya.

Aidha amesema agizo hilo pia liendane na suala la kudhibiti shughuli zote za kibinadamu kando kando ya mita 60  kwa kufuata sheria ya mita 60.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Mbeya ametoa agizo hilo katika kilele cha upandaji  miti kimkoa katika eneo la chanzo cha maji cha mto Hanzya kata ya Itagano jijini Mbeya.

Amesema lazima agizo hilo litekelezwe mapema sanjali na kufanya tathimini ya hali yauhalibifu wa  mazingira katika maeneo yot.


"Nikazi bure kuendelea kupanda miti wakati ile iliyopandwa mwaka uliopitwa imehalibiwa kwa kukosa matunzo au kuhalibiwa kwa shughuli za kibInadam"Alisema Makala.


Aidha Makalla ameitaka jamii kujenga utamaduni wa kupanda miti ya vivuli na matunda kwenye maeneo yao hususani katika maeneo ya vyanzo vya maji  kwani ni muhimu kwa maisha ya kila siku.


 "Serikali imeweka lengo la kupanda miti isiyopungua milioni 1 kwa mwaka  katika kila halmashauri mkoani humo  ambapo mwezi juni mwaka huu  kufanyika tathimini ya pamoja kuona zoezi hilo lilipo fikiwa"Alisema .


Naye Afisa Misitu Mkoa wa Mbeya Ndugu Joseph Butuyuyu mpango wa kuhifadhi safu ya Mlima Mbeya umeanza kwa mafanikio makubwa hasa kutokana kuungwa mkono na waziri mwenye dhamana ya Mazingira Ndugu January Makamba mara baada ya kutembelea safu ya Mlima huo.
Mwisho

Wananchi wa kijiji cha Hanzya kata ya Itagano wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla katika kilele cha Upandaji Miti Kimkoa katika SAFU ya Mlima Mbeya January 31 ,2017

Afisa habari na Mawasiliano Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira jijini Mbeya (UWSA)akichukua matukio katika tukio hilo la kilele cha upandaji miti kimkoa katika safu ya Mlima Mbeya Itagano.

Mkutano ukiendelea.........

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akipanda mti katika kilele cha Upandaji kimkoa katika chanzo cha Maji Hanzya Kata ya Itagano.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla kushoto akiteta jambo na Meya wa jiji la Mbeya David Mwashilindi mara baada ya kumaliza zoezi la upandaji miti katika Safu ya Mlima Mbeya eneo la Chanzo cha maji cha Hanzya kata ya Itagano jijini Mbeya

Askari wa JKT Itende Mbeya pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira jijini Mbeya (UWSA) na baadhi ya watumishi halmashauri ya jiji la Mbeya wakiendelea na zoezi la upandaji miti katika Safu ya Mlima Mbeya katika Chanzo cha Maji Hanzya Itagano Jijini Mbeya .Picha Fahari News na JamiiMojablog.

No comments: