Thursday, December 31, 2015

Waziri Mahiga akutana na Mabalozi wa Qatar na Kuwait waliopo nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akifanya mazungumzo na Balozi wa Qatar Mhe. Abdullah Jassim Almaadadi alipofika Wizarani kwa ajili ya kumpongeza kwa kuteuliwa katika wadhifa wake mpya na pia kumhakikishia ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar. Mazungumzo hayo yalifanyika tarehe 30 Desemba, 2015. 
Balozi Al maadadi naye akizungumza huku Mhe. Mahiga akimsikiliza. 
Mazungumzo yakiendelea 
Waziri Mahiga akiagana na Balozi Al Maadadi mara baada ya kumaliza mazungumzo. 
.......Mkutano na Balozi wa Kuwait nchini 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Nassem Ibrahim Al Najib, alipokuja kumtembelea Wizarani na kufanya mazungumzo naye kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait na pia kumpongeza. 
Balozi Mahiga akiagana na Balozi wa Kuwait mara baada ya kumaliza mazungumzo naye. 
Picha na Reginald Philip

No comments: