Saturday, January 31, 2015

CHIPUKIZI WA UVCCM WAJIFUA VIKALI TAYARI KWA KILELE CHA MIAKA 38 YA CCM KESHO

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Mratibu wa Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM, Emmanuel Nchimbi, walipokuwa wakikagua mazoezi ya vijana wa Chipukizi wa CCM ya paredi na halaiki kwa ajili ya Maadhimisho ya Kilele cha Miaka 38 ya CCM, yatakayofanyika Kitaifa kesho kwenye Uwanja wa majiMaji mjini Songea.
 Vijana wa Chipukizi wa CCM waliopo katika mazoezi ya halaiki na paredi kwa ajili ya Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM mjini Songea, wakikipiga saluti wakati wa mazoezi ya mwisho leo kwenye uwanja wa Majimaji
 Kijana wa Chipukizi wa CCM Mbaraka Ngonyani akionyesha umakini wake wakati akipiga saluti wakati wa mazoezi hayo ya mwisho leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa  UVCCM Sixtus Mapunda wakitazama mazoezi ya mwisho ya Chipukizi hao
 Mshika bendera ya CCM kwenye kikosi cha Bendera cha Gwaride la Umoja wa Vijana wa CCM, Sharif Mohammed na wenzake wakipita kwa ukakamavu mbele ya jukwaa kuu wakati wa mazoezi ya mwisho ya gwaride na halaiki kwa ajili ya Kilala cha Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM yanayofanyika kesho Kitaifa kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea mkoani Ruvuma 
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha mazoezi ya ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wakionyesha ohodari wao wa mazoezi ya 'kikomandoo' wakati wa mazoezi yao ya mwisho ya paredi na halaiki kwa ajili ya kilele cha maadhimisho ya miaka 38 ya CCM kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Chipukizu hao wakiwa kwenye mazoezi ya halaiki
Mmoja wa Chipukizi wa CCM waliokuwa katika mazoezi hayo akisaidiwa baada ya kuanguka kutokana na mazoezi hayo ya mwisho kupamba moto. Alipata ahueni baada ya kupatiwa huduma ya kwanza. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

1 comment:

Simeon Corneli Mwakatobe said...

Kichekesho miaka 50 ya uhuru na maenedeleo bado chipukizi wa UVCCM hawavai viatu! Kulikoni wahusika kutowezesha hata viatu vya matairi ili kujikinga na kokoto?