Friday, January 31, 2014

Ubalozi wa China watoa msaada kwa waathirika wa mafuriko mkaoni Morogoro

Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Lu Youping akikabidhi msaada wa vifaa mbalimbali kwa Mkurugenzi wa Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Leteni Jenerali Sylivester Rioba. msaada huo ambao unathamani ya Shilingi milioni 32 umetolewa kwa ajili ya watu walioathirika na mafuriko mkoani Morogoro.
Balozi wa China (katikati) akishikana mikono na Luteni Generali Rioba na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Athony Mtaka wakati wa hafla ya kukabidhi msaada iliyofanyika katika Ubalozi wa China. nyuma yao lori aina ya fuso likiwa limejazwa baadhi ya bidhaa za msaada huo.
Balozi wa China akikabidhi stakabadhi za vifaa vya msaada kwa Leteni Jenerali Rioba huku Mkuu wa Wilaya ya Mvomero akishuhudia.
Wanahabari nao hawakuwa mbali kushuhudia hafla ya makabidhiano.
Balozi wa China, Mhe. Lu Youping akitoa hotuba fupi.
Mkurugenzi wa Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu akitoa hotuba ya kushukuru msaada uliotolewa na Balozi wa China.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mberwa Kairuki akisalimiana na Luteni Jenerali Rioba mara baada ya hafla ya kukabidhi misaada kukamilika. Picha na Reginald Philip Kisaka.

No comments: